Tuesday, December 29, 2009

KIFIMBO KILIPOTUA IKULU KWA JK


MBIO ZA KIFIMBO CHA MALKIA KATIKA PICHA


Wavuvi nao katika Soko la Samaki Magogoni hawakuwa nyuma...

Utamaduni wa wahindi haukuachwa nyuma...

Rais wa TFF, Leodgar Tenga na Mkurugenzi wa TBC, Tido Muhando hawakuachwa nyuma...

Maafande wetu si tu wanapambana na wahalifu, lakini hata katika shughuli za kijamii wamo...

Tabasamu la Kifimbo cha Malkia...

Friday, December 25, 2009

KILAINI ATOA SOMO KUSHEREHEKEA KRISMASI

Aliyekuwa Askofu Mkuu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Methodius Kilaini amewaasa wazazi na walezi kusherehekea pamoja na familia zao Sikukuu ya Krismasi ambayo imeadhimishwa leo duniani kote na waumini wa dini ya Kikristo.

Kilaaini amesema ni vema kama unakwenda kusherehekea mbali na nyumbani ukabeba familia yako yote na si kuiacha nyingine ikiwa wapweke kwa kushindwa kusherehekea sikukuu hii.

Askofu Kilaini ametoa kauli hiyo wakati wa Ibada ya Misa ya Krismasi iliyofanyika kitaifa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam leo asubuhi.


Askofu Kilaini akizungumza na mtoto

Wednesday, December 9, 2009

TANZANIA YAADHIMISHA MIAKA 48 YA UHURU


Watoto wa Halaiki wakijipanga katika mistari iliyonyooka katika kuadhimisha Miaka 48 ya Uhuru wa Tanzania leo katika Uwanja wa Uhuru, jijini

Thursday, December 3, 2009

HAPA VIPI?


Kondakta wa dalada linalofanya safari zake kati ya Kimara na Kariakoo akipakia abiria sehemu ya kivuko cha watembea kwa miguu, Njia panda ya Mabibo, Urafiki. Hii si mara ya kwanza kwa makondakta na madereva wao kupakia na kushusha abiria sehemu hii jambo ambalo ni ukiukaji wa sheria za usalama barabarani.... Kamanda Kombe upo?