Friday, December 25, 2009

KILAINI ATOA SOMO KUSHEREHEKEA KRISMASI

Aliyekuwa Askofu Mkuu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Methodius Kilaini amewaasa wazazi na walezi kusherehekea pamoja na familia zao Sikukuu ya Krismasi ambayo imeadhimishwa leo duniani kote na waumini wa dini ya Kikristo.

Kilaaini amesema ni vema kama unakwenda kusherehekea mbali na nyumbani ukabeba familia yako yote na si kuiacha nyingine ikiwa wapweke kwa kushindwa kusherehekea sikukuu hii.

Askofu Kilaini ametoa kauli hiyo wakati wa Ibada ya Misa ya Krismasi iliyofanyika kitaifa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam leo asubuhi.


Askofu Kilaini akizungumza na mtoto

No comments:

Post a Comment