'JK' aliwapasha maofisa hao mbele ya 'wapiga kura' wake katika maeneo tofauti tofauti na kwa nyakati tofauti alipofanya ziara katika maeneo hayo kuangalia maendeleo ya upatikanaji wa Majisafi kwa wananchi hao ikiwa ni ziara yake maalumu jijini hapa.
"Hawa ndiyo wanaowalalimikieni na si mimi. Wasikilizeni wanataka nini na muwatimizie, vinginevyo hawatawaelewa hawa!!" Aliwaambia maofisa hao na kuongeza, "Watekelezeeni mahitaji yao na muwache blaa blaa..." Alisema huku akishangiliwa na mamia ya wananchi hao waliofurika katika maeneo hayo tofautitofauti.
PICHA ZAIDI
Rais Kikwete akihutubia
Sehemu ya wananchi waliofurika kumshuhudia Rais Kikwete
Rais Kikwete akiongea na watoto wa chekechekea ya Gift ya Keko