Sunday, May 23, 2010

TWIGA STARS MPANGO MZIMA! YAICHAPA ERITREA 8-1

Timu ya Taifa ya wanawake 'Twiga Stars' leo imefanikiwa kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika kwa wanawake baada ya kuinyuka Eritrea kwa jumla ya magoli 8-1.

Mwanahamisi Omary na Asha Rashidi waling'ara uwanjani baada ya kila mmoja kuondoka na kapu la magoli ya kutosha, ambapo Mwanahamisi aliondoka na magoli manne huku Asha akiondoka na magoli 3.

Kwa matokeo hayo, Twiga Stars itacheza mchezo wa marudiano dhidi ya timu hiyo Eritrea mjini Asmara.


Wachezaji wa Twiga Stars wakishangilia baada ya kumalizika kwa mchezo

Mwanahamisi Omary 'Redondo' (juu) akiruka kihunzi cha beki wa Eritrea, Semhar Bereket Bhabla

PICHA ZAIDI

Warembo wanaoshiriki shindano la Miss Dar Inter-College wakiwa katika picha ya pamoja na kipa no.1 Fatuma Omary

Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika akizungumza na wandishi wa habari baada ya pambano

Makipa wa Twiga (kulia na Kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na mrembo

Kipa namba 1 Fatuma Omary akiwa katika picha ya pamoja na warembo

No comments:

Post a Comment