Monday, May 24, 2010

JK AWAPASHA MAOFISA WA DAWASA, EWURA LIVE

Rais Jakaya Kikwete kama ilivyo kawaida yake ya kuwatolea uvivu watendaji wasiowajibika kwa wananchi wao, leo amewapasha maofisa wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka jijini (DAWASA) na wale wa Mamlaka inayodhibiti Maji na Nishati (EWURA) 'live' bila chenga kwa kuwaambia waache ubabaishaji na blablaa badala yake wawe watendaji zaidi.

'JK' aliwapasha maofisa hao mbele ya 'wapiga kura' wake katika maeneo tofauti tofauti na kwa nyakati tofauti alipofanya ziara katika maeneo hayo kuangalia maendeleo ya upatikanaji wa Majisafi kwa wananchi hao ikiwa ni ziara yake maalumu jijini hapa.

"Hawa ndiyo wanaowalalimikieni na si mimi. Wasikilizeni wanataka nini na muwatimizie, vinginevyo hawatawaelewa hawa!!" Aliwaambia maofisa hao na kuongeza, "Watekelezeeni mahitaji yao na muwache blaa blaa..." Alisema huku akishangiliwa na mamia ya wananchi hao waliofurika katika maeneo hayo tofautitofauti.

PICHA ZAIDI

Rais Kikwete akihutubia



Sehemu ya wananchi waliofurika kumshuhudia Rais Kikwete

Rais Kikwete akiongea na watoto wa chekechekea ya Gift ya Keko

No comments:

Post a Comment