Thursday, July 29, 2010

SAFARI YA MWISHO YA PRIMTIVA PANCRAS...

Na Primtiva Pancras...,
Hivi ndivyo nilivyozoea kuona BY LINE yake mara kwa mara ninapolisoma gazeti la Mtanzania linalochapishwa na Kampuni ya New Habari.

Ama kwa hakika, 'Prim' kama wengi tulivyozoea kumwita wakati wa uhai wake, alikuwa ni rafiki wa kila mmoja wetu. Hakuna unafiki hapa wa kusubiri mpaka mtu afariki ndo mazuri yake yatangazwe. Kwa aliyemjua 'Prim' hatotia shaka wala kuguna kwa hili nalonena.

Prim, alikuwa hodari wa kazi. Kwa sisi ambao mara moja moja tunakuwa na vijikazi vya hapa na pale, hupenda kuita wanataaluma wenzetu kwa ajili ya kusaidiana. Prim hakusita kuja pindi unapomuita kwenye kazi yako. Na kama hatokuwa na nafasi basi atamtuma mtu mradi tu kazi yako isilale.

Prim ana mengi ya kumzungumzia, ambayo unaweza kutumia siku nzima kuyaandika, lakini kwa kifupi, ndo hayo, Na hii ndiyo Safari ya Mwisho ya Primtiva... Mungu amrehemu sana, Amin.

MAZISHI YAKE PICHANI

Primtiva enzi za uhai wake


Waandishi wakimuaga Primtiva Kanisa la Roman la Hananasif


Mchungaji akifukiza udi kwenye jeneza la Primtiva


Sanduku la Primtiva likishushwa kaburini kwa maziko


Joachim Mushi akimwaga mchanga kwenye kaburi la mke wake, Primtiva

No comments:

Post a Comment