Tuesday, September 14, 2010

WASAJILI WAPYA WA MAHAKAMA KUU WAAPISHWA LEO


Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Fakihi Jundu (katikati mbele), Jaji Mfawidhi wa Mahakama ya Ardhi, Regina Rweyemamu (wa pili kulia) na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Dar es Salaam, Semistocles Kaijage (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wasajili wapya wa Mahakama Kuu Tanzania walioapishwa leo

KAMPENI DAR ZADORORA, MIKOANI MBELE KWA MBELE

Wakati kampeni za uchaguzi zikiwa zinapata hamasa zaidi huko mikoani, huku jijini Dar tunashuhudia zikiwa zimedorora.

Utafiti unaonesha kuwa wakazi wa jiji hili wamekuwa wakibanwa na majukumu yao binafsi zaidi ukilinganisha na maeneo ya mikoani ambako wengi wa wananchi wa huko wamekuwa wakiacha shughuli zao kwa muda na kujitokeza kwa wingi kwenye mikutano ya kampeni.

Mbali na hilo, pia hamasa zaidi katika kampeni za awamu hii ipo mikoani zaidi kutokana na wagombea wengi kuwa wapya ambao wameonesha kuchuana zaidi ukilinganisha na awamu iliyopita.

KAMPENI PICHANI LEO:

JK: BUMBULI





SALMA KIKWETE: MUSOMA




JUMA DUNI HAJI WA CUF: SUMVE



DK BILAL: DODOMA


TICTS WATIMIZA MIAKA 10 YA MAFANIKIO

Kampuni ya kuhudumia makontena bandarini (TICTS) jana imetimiza miaka 10 tangu kuanza kutoa huduma zake hapa nchini huku ikiwa imebadilisha taswira ya awali iliyokuwepo kwenye bandari zetu nchini.



Waziri wa Miundombinu Dk Shukuru Kawambwa anasema kuwa hali ya upakuaji makontena kwenye bandari zetu kabla kampuni hiyo haijaanza kuendesha shughuli zake hapa nchini ilikuwa si yakuridhisha ukilinganisha na sasa. "Tunaiombea iendelee kuleta mabadiliko mpaka kufikia mwaka 2025." Alisema.

Katika kuhakikisha shughuli za upakuaji makontena kwenye bandari zetu zinaboreshwa, jana kampuni hii imezindua winchi mpya moja yenye kasi na uwezo wa kubeba makontena mawili kwa wakati mmoja na kufanya idadi ya winchi nne yaani 'cranes'.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa TICTS, Neville Bissett amewaambia waandishi wa habari pamoja na wadau waliohudhuria hafla hiyo jana Dar es Salaam kuwa kampuni yake kwa kushirikiana na vitengo mbalimbali vinavyotoa huduma bandarini hapo ikiwemo TRA, inaendelea kuboresha utendaji kazi wake ili kumaliza kabisa tatizo la mlundikano wa makontena.



Amewatoa hofu wateja wanaotumia bandari hiyo na kuwahakikishia mabadiliko ya hali ya juu zaidi. "Tumeboresha shughuli zetu ukilinganisha na tulivyoanza. Uwezo wetu umekuwa mkubwa kwa kuongeza winchi mpya na za kisasa zaidi." Alisema.

Saturday, September 4, 2010

Thursday, September 2, 2010

HEALTHIER DISABILITIES


A doctor with an Indian Navy examines girl with a disability at Uhuru co-education recently. A girl is a deaf and eyes disability.

NYAMISATI NA HAZINA ILIYOFICHIKA

Nyamisati ni kijiji kilichopo kilometa 42 toka barabara kuu iendayo Lindi na Mtwara. Kijiji hiki kipo katika wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Asilimia kubwa ya wakazi wa eneo hili ni wa kabila la wandengereko. Kijiji hiki kipo ufukweni mwa delta ya mto Rufiji unaotiririsha maji yake kwenye bahari ya Hindi. Hivyo basi utagundua kuwa uvuvi kijijini hapo ni moja ya shughuli zinazofanywa na wakazi wa kijiji hicho.



Pia, aina ya samaki wanaovuliwa Nyamisati ni aghalabu sana kupatikana Dar es Salaam kutokana na sababu ya kijiografia ya eneo hilo. Kamba ni miongoni mwa bidha inayovuliwa kwa wingi na wavuvi, wakazi wa Nyamisati na kuwasafirisha maeneo jirani na sehemu hiyo, ikiwemo Dar es Salaam.

Kamba hawa wanaovuliwa Nyamisati ni wa aina mbili, kamba wadogo 'Prons' na kamba wakubwa 'Lobsters'. Lobster mmoja wakati mwingine hufikia mpaka kilo 4. Na hii ina maana kwamba hata uvuvi wake ni tofauti na kamba wadogo 'Pons'.

Kilichonistajabisha ni kwamba, mbali na kupatikana kwa wingi kwa bidhaa hiyo ya kamba eneo hilo la Nyamisati, bado kuna changamoto ya soko la kuhifadhia bidha hao. Hii inasababisha uvuvi wa kamba hao unaofanyika Nyamisati kuwa ni mdogo na wa kubahatisha ukilinganisha na sifa yake.

USAFIRI WA MAJINI
Mitumbwi na boti ni nyenzo muhimu za usafiri kwa wakazi waishio vijiji jirani vilivyopo ng'ambo na Nyamisati. Mbali na wakazi wa vijiji jirani na Nyamisati, bali pia hata wakazi waisho kisiwa cha Mafia pia hutumia Nyamisati kama bandari muhimu kwa ajili ya kusafirisha bidhaa zao na huduma nyinginezo.


Wakazi wa Nyamisati wakiwa na bidhaa zao wakisafiri kwa boti


Wakazi wa Nyamisati wakisafiri kwa boti

"Mwendo wa kutoka hapa mpaka Mafia ni kama masaa matatu mpaka mawili na nusu." Anasema mmoja wa wakazi wa Nyamisati.