Thursday, September 2, 2010

NYAMISATI NA HAZINA ILIYOFICHIKA

Nyamisati ni kijiji kilichopo kilometa 42 toka barabara kuu iendayo Lindi na Mtwara. Kijiji hiki kipo katika wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Asilimia kubwa ya wakazi wa eneo hili ni wa kabila la wandengereko. Kijiji hiki kipo ufukweni mwa delta ya mto Rufiji unaotiririsha maji yake kwenye bahari ya Hindi. Hivyo basi utagundua kuwa uvuvi kijijini hapo ni moja ya shughuli zinazofanywa na wakazi wa kijiji hicho.



Pia, aina ya samaki wanaovuliwa Nyamisati ni aghalabu sana kupatikana Dar es Salaam kutokana na sababu ya kijiografia ya eneo hilo. Kamba ni miongoni mwa bidha inayovuliwa kwa wingi na wavuvi, wakazi wa Nyamisati na kuwasafirisha maeneo jirani na sehemu hiyo, ikiwemo Dar es Salaam.

Kamba hawa wanaovuliwa Nyamisati ni wa aina mbili, kamba wadogo 'Prons' na kamba wakubwa 'Lobsters'. Lobster mmoja wakati mwingine hufikia mpaka kilo 4. Na hii ina maana kwamba hata uvuvi wake ni tofauti na kamba wadogo 'Pons'.

Kilichonistajabisha ni kwamba, mbali na kupatikana kwa wingi kwa bidhaa hiyo ya kamba eneo hilo la Nyamisati, bado kuna changamoto ya soko la kuhifadhia bidha hao. Hii inasababisha uvuvi wa kamba hao unaofanyika Nyamisati kuwa ni mdogo na wa kubahatisha ukilinganisha na sifa yake.

USAFIRI WA MAJINI
Mitumbwi na boti ni nyenzo muhimu za usafiri kwa wakazi waishio vijiji jirani vilivyopo ng'ambo na Nyamisati. Mbali na wakazi wa vijiji jirani na Nyamisati, bali pia hata wakazi waisho kisiwa cha Mafia pia hutumia Nyamisati kama bandari muhimu kwa ajili ya kusafirisha bidhaa zao na huduma nyinginezo.


Wakazi wa Nyamisati wakiwa na bidhaa zao wakisafiri kwa boti


Wakazi wa Nyamisati wakisafiri kwa boti

"Mwendo wa kutoka hapa mpaka Mafia ni kama masaa matatu mpaka mawili na nusu." Anasema mmoja wa wakazi wa Nyamisati.

No comments:

Post a Comment