Tuesday, November 16, 2010

PINDA NDIYE WAZIRI MKUU


Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda amemtangaza Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano iliyobaki.

Spika Makinda alimtaja Mheshimiwa Pinda kuwa Waziri Mkuu baada ya kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kupitia waraka wake aliomuandikia spika huyo na kusomwa mbele ya wabunge wa bunge hilo leo jioni.

"Nachukua fursa hii kumtangaza Mizengo Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania." Alisema spika Makinda wakati akisoma barua hiyo iliyotumwa kwake.

No comments:

Post a Comment