Sunday, November 7, 2010

MAJERUHI CHENGE ATANGAZA KUGOMBEA USPIKA



Mbunge mteule wa Jimbo la Bariadi Magharibi, Andrew Chenge ametangaza azma yake ya kugombea bafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Dar es Salaam.

Chenge ametangaza azma yake hiyo mbele ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini alipofanya nao mkutano kwenye hoteli ya Courtyard, eneo la Upanga Sea view, majira ya saa sita mchana.

"Nimewaita hapa leo ndugu zangu kwa lengo moja tu la kutangaza azma yangu ya kugombea nafasi ya Uspika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili niweze kutibu majeraha makubwa yaliyoumiza Bunge, Taifa na wananchi wa chama changu (CCM). Mimi kama ilivyo kwa wengine ni miongoni mwa majeruhi wa uongozi, Kama bunge, hatuna budi kukabiliana nalo kwa nguvu kubwa." alisema na kuongeza,

"Bunge letu limekuwa na changamoto kubwa katika miaka mitano iliyopita. Viongozi ambao wajibu wetu ni kuonesha njia badala yake tumekuwa vinara wa uzushi, uongo, fitna na majungu. Mimi ni mwarobaini (dawa ya kutibu) wa majeraha hayo, ambaye naamini ni kiongozi bora na nina uwezo na nia thabiti." Alisema

No comments:

Post a Comment