Monday, November 15, 2010

WANAJESHI WA UINGEREZA WATOA MAFUNZO YA KUPAMBANA NA MAHARAMIA KWA WANAJESHI WA TANZANIA

Askari wa Jeshi la wanamaji wa Uingereza wamo nchini kwa siku tano ambapo wataendesha mafunzo ya kijeshi kwa askari wa jeshi la wanamaji hapa nchini ya namna ya kupambana na maharamia.

Askari hao waliowasili kwenye Bandari ya Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kwa meli ya kivita ya HMS Montrose watakuwepo kwa siku tano kabla ya kuondoka, ambapo vikosi mbalimbali vya wanamaji wa Tanzania vitapewa mbinu na mafunzo ya namna ya kupambana na maharamia.

Wakiwa njiani kuja hapa nchini, askari hao wameweza kudhibiti maharamia wa somalia kwa kiwango kikubwa. Kamanda wa meli hiyo, Jonathan Lett anasema, "Tumeweza kudhibiti kwa kiasi kikubwa maharamia katika pwani ya Somalia." Alisema.



British Royal Navy soldier, Rob McMurrich with his General Purpose Machine Gun

No comments:

Post a Comment