Monday, June 1, 2009

Liyumba kuendelea kusota Mahabusu

Mtuhumiwa wa kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia hasara Serikali ya zaidi ya bilioni 200, Amatus Liyumba amerudishwa tena mahabusu baada ya dhamana yake kugonga mwamba kutokana na kushindwa kutimiza masharti yake mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Ngigulila Mwaseba.

Liyumba na mawakili wake waliwasilisha vivuli vya hati ya mali ambavyo mahakama ilitupilia mbali ombi hilo, na kuhitaji hati halisi, na hivyo Hakimu kuamuru Liyumba kurudishwa mahabusu mpaka tarehe 15 ya mwezi juni kwa ajili ya kusikiliza tena maombi hayo ya dhamana.

SOURCE: Neema Mgonja


Liyumba (kushoto) akiteta jambo na wakili wake, Majura Magafu...

No comments:

Post a Comment