Monday, June 1, 2009

Waathirika wa mabomu waomba kuhamishwa

Wakazi wa Mbagala, waathirika wa milipuko ya mabomu wameitaka Serikali kuwahamisha eneo hilo kwa madai kuwa usalama wa maisha yao upo hatarini.

Mmoja wa wakazi hao, aliyejitambulisha kwa jina la Mama Jacky amesema kuwa tangu walipoanza kuishi maisha ya kambini, afya zao pamoja na za watoto zimekuwa zikiathirika siku hadi siku kutokana na mazingira yaliyopo eneo hilo.

Amesema kuwa, wakati mwingine wanalazimika kuyahama makazi yao kwa muda inapotokea taarifa kuhusu kulipuliwa kwa mabomu mengine, jambo linalowafanya kuishi maisha ya wasiwasi.

"Zamani Kilungule nilikuwa napaona mbali sana ukilinganisha na siku hizi ambapo napaona ni karibu hasa kunapokuja taarifa za kulipuliwa kwa mabomu. Huwa nakimbia mpaka huko." Alisema Mama Jacky.


Mkazi wa Mbagala akionyesha nyumba yake ilivyoteketezwa kwa mabomu...

No comments:

Post a Comment