Friday, October 29, 2010

BEACH ZETU CHAFU!!

Huu ni ufukwe na wala si dampo. Eneo hili ni maarufu sana hapa mjini ambalo mwisho wa wiki wananchi hupendelea kwenda kujipumzisha na wengine kuoga kwa ajili ya kupunguza joto la jiji hili.



Eneo hili ni Ufukwe wa Coco almaarufu 'Coco Beach'. Lakini mandhari inayoonekana hapa haivutii kutokana na taka bahari zilizolundikana.

Je, kwa hali hii kuna ulazima wa kuendelea kuwapigia kelele wawekezaji wa kigeni kuwa wanatunyima wazalendo fursa za kufanya biashara? Mfano ufukwe huu ungekuwa chini ya mwekezaji wa kigeni unadhani hali ingekuwaje?

Tufanye kazi watanzania wenzangu na tuache kubweteka kwani mafanikio hayaji kiurahisi rahisi tu!

No comments:

Post a Comment