Friday, October 29, 2010

DINI-VIONGOZI WA DINI WAUSIA UCHAGUZI WA AMANI

Viongozi wa dini leo wamefanya ziara kwenye vyama mbalimbali vya siasa kuhimiza Uchaguzi wa amani nchini.

Wakiwa kwenye Makao Makuu ya Chama cha Wananchi (CUF), viongozi hao wamesisitiza uchaguzi wa haki ili wananchi wawapate wale viongozi waliowachagua na si vinginevyo.



"Hata vitabu vya dini vinakemea dhuluma ya haki, kila mwana adamu ana haki ya kuchagua akipendacho." Alisema Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum.



Naye Askofu Mkuu wa Baraza la Maaskofu nchini (TEC), Paul Rukoza amesema kuwa wananchi wanatakiwa kujifunza ustahamilivu wakati wakupokea matokeo. Amesema kuwa wakati wa kmapeni kila upande hujiamini kupita kawaida kutokana na maandalizi jambo ambalo mwisho wa siku huweza kuibua malumbano na machafuko na kuathiri mfumo wa maisha.

"Hata hivyo tunapenda kuviasa baadhi ya vyombo vya habari vyenye mitazamo hasi kuhusu mikutano yetu sisi viongozi wa dini." Alisema

No comments:

Post a Comment