Friday, October 29, 2010

MATUNDA BWERERE, WAPI VIWANDA?

Tanzania imejaaliwa kwa kuwa na ardhi yenye kukubali kila aina ya zao. Matunda ni miongoni mwa mazao yanayostawi vizuri kwenye ardhi ya nchi hii. Unapofika msimu wake, matunda huwa ni mengi sana kwenye masoko yetu 'local markets'.

Huruma huwa inanijia pale ninapoona matunda hayo yanapokuwa mengi kwenye masoko yetu na kukosa wanunuzi ambapo mwisho wa siku huwa yanaoza, kuharibika kabisa mikononi mwa wafanyabiashara.



Wapi viwanda vya usindikaji wa matunda haya? Wapi viwanda vya kutengeneza 'juisi' za matunda haya? Matunda kama Machungwa, Maembe, Mananasi na mengineyo?

Kwanini Kenya waweze, sisi tushindwe? Kwa nini? Mchawi ni nani? Ona pichani ndizi hizi mbivu kwenye Soko la Buguruni zilivyolundikana hapo chini zikitafuta wanunuzi!! Baada ya siku chache pita tena hapohapo sokoni utaona namna ndizi hizo zilivyo ozeana, kulaliana na kupondekapondeka!

No comments:

Post a Comment