Tuesday, March 29, 2011

DK BILAL AKAGUA MASHAMBA YA MPUNGA YA MTO WA MBU

Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal leo ameingia kwenye siku ya tatu ya ziara yake katika mkoa wa Arusha ambapo anatembelea miradi mbalimbali kwa lengo la kuikagua pamoja na kuizindua mingine.

Miongoni mwa miradi aliyoizindua ni pamoja na ujenzi wa Maabara ya Shule ya Sekondari ya Nanja, wilayani Monduli.

Leo Dk Bilal ametembelea mashamba ya mpunga yaliyopo kwenye mabonde ya mto wa Mbu, wilayani Monduli pamoja na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la maabara ya Shule ya sekondri Nanja, wilayani Monduli. Zifuatazo ni picha mbalimbali zinazoonyesha matukio hayo:



Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal akiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirima kukagua mashamba hayo



Dk Bilal akiangalia mashamba hayo



Dk Bilal akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la maabara ya shule hiyo. Wa mwisho kabisa ni Mbunge wa wilaya hiyo, Edward Lowassa

No comments:

Post a Comment