Tuesday, March 29, 2011

NEMC YATOA MILIONI 15 KWA VIKUNDI VYA MAZINGIRA

Baraza la Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC), leo asubuhi limekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 15 kwa vikundi vya mazingira kutoka mikoa mitatu ya Kilimanjaro, Mara na Morogoro kwa ajili ya kusaidia kuendeleza miradi ya mazingira katika maeneo yao.

Vikundi hivyo ni Angaza Women cha Siha mkoani Kilimanjaro, Watu Maji na Mazingira (WAMAMA) cha Tarime mkoani Mara pamoja na Kilombero Group for Community Development (KGCD) ambavyo kila kimoja kimepata shilingi milioni 5.


Wawakilishi wa vikundi hivyo, (Kutoka kushoto) Christina Kulunge wa Morogoro, Lucas Bwana wa Tarime na Mama Mchungaji Joyceline Njama wa Kilimanjaro kwa pamoja wakiangalia mfano wa hundi yao waliyokabidhiwa leo na NEMC

No comments:

Post a Comment