Monday, August 1, 2011

LAGHAI MZOEFU ANASWA MTAA WA KONGO

Usithubutu kusimamisha gari lako pindi akufuatapo na kuanza kukwambia umemgonga! Kitakachofuatia ni kukupora kila kitu kilichomo kwenye gari lako. Huyu ni laghai mzoefu aliyekuwa amefumbiwa macho na wafanyabiashara wa Mtaa wa Kongo jijini Dar es Salaam aliyefahamika kwa jina moja la Nurdin. Lakini waswahili wanasema za mwizi arobaini. Leo amenaswa kweupeee na mgambo wa jiji akitaka kumlaghai dereva wa teksi mtaani hapohapo! Fuatilia tukio zima katia 'series' ya picha


Ilianza hivi... Hawa ni Mgambo wa jiji wapo kwenye Patrol yao...


Ghafla wanamkuta 'Nurdin' akiwa amemzuia dereva wa teksi akidai kagongwa...


Mgambo wanashuka ili kujua nini kinachoendelea...


Mgambo baada ya kuhoji na kuambiwa 'Nurdin' ni laghai na ndio staili zake, wanamkwida na kuondoka naye...


Wanamdhibiti kisawasawa ili kumpandisha kwenye gari lao...


'Nurdin' anapingana nao na kuanza kuleta kashkash...


Lakini nguvu ya 'Teja Nurdin' ni ya kitoto sana kwa mgambo hawa... wanampandisha sasa kwenye gari lao...


Hapa amedhibitiwa kisawasawa akiwa ndani ya gari la mgambo hawa...


Hebu 'cheki' sura hii ukiambiwa ni kibaka na tapeli mzoefu utakataa? Mgambo haoooo wanaondoka na Nurdin...

No comments:

Post a Comment