Thursday, April 29, 2010

ROBI MORRO AND JAMILA VERA SWAI LAUNCH THEIR READY TO WEAR COLLECTION

Inaugural “Origin Africa Designer Showcase” was held last night on 28 April 2010 in Nairobi at the Laico Regency which saw two Tanzanian Swahili Fashion Week designers Robi Morro and Jamilla Vera Swai Launch their new collection.

Tanzania Cotton Board’s (TCB) Textile Sector Development Unit (TSDU) – through the
Organisers’ of the Swahili Fashion Week – had facilitated the participation of Robi Morro and Jamilla Vera Swai.

The work of the Textile Sector Development Unit has been made possible by support from the Gatsby Charitable Foundation and its associated Tanzania Gatsby Trust (TGT). Tanzania Cotton Board wants to ensure that more Tanzanian grown cotton is transformed into higher value added products in Tanzania

Robi Morro of Mapozi Designs collection is named Garden of Style , which is inspired by the woman.” A woman is like a flower, she blossom well if taken good care of” said Robi. “The pieces are very feminine, flirty, sassy colourful and fun aimed at bringing out the woman's beauty with the use of bold colourful floral prints.” added Ms Morro

Jamila’s Collection is named “Say and Color Zero” Inspired by her daughter of two first school homework “Say and Color Zero”. This became her constant routine for every evening. “Her favourite colors being red and black, I decided working with that by layering them by individual colors, with the print zero” said Jamilla.

Wednesday, April 28, 2010

ZIARA YA ARUSHA NA MOSHI PICHANI


Maporomoko ya Maji katika Kijiji cha Chomvu, Usangi


Hii ndiyo nyumba ya Waziri Mkuu wa zamani, Cleopa Msuya


ZIwa Jipe linavyoonekana kutokea milima ya Usangi.


Ua hili sikuweza kulifahamu mara moja. Nililikuta meneo ya Kibosho, milimani huko


Huu ni ukungu ambao nilikutana nao maeneo ya Mweka, ni milimani kabisa huko..

Shortly, Arusha, Moshi na Mwanga nilikwenda kutembelea miradi ya Maendeleo ya Jamii inayofadhiliwa na Serikali. Kiujumla wananchi wenye miradi hiyo wamenufaika na hali zao kimaisha zimebadilika ukilinganisha na awali.

Wengine awali walikuwa wakishindia mlo mmoja kwa siku ukilinganisha na sasa hivi ambapo kwa siku wanapata mlo mara tatu. Hata ukiangalia afya zao ni nzuri na wana nyuso zenye nuru.

Kesho nitawaletea mfululizo wa kila ziara na mradi wake, pamoja na mahojiano na kila mlengwa wa mradi huo..

Thursday, April 15, 2010

REX INVESTMENT KUPELEKA UMEME WA JUA VIJIJINI...


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Wakandarasi wa Nishati ya Jua ya Rex Investment Limited, Francis Kibhisa (kushoto) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya Nishati ya Jua ya Megawatt 1 toka Kampuni ya SUNTECH ya nchini China leo Dar es Salaam. Mwingine ni Meneja Mauzo wa SUNTECH, Vincent Song. Mpango huo utalenga zaidi kusaidia maendeleo ya wananchi wa vijijini

BAADA YA MASOMO NI WAKATI WA KULA MATUNDA...


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Dar es Salaam wakichagua matunda aina ya 'Apples' kwa ajili ya kununua leo mchana nje ya shule hiyo iliyopo eneo la Gerezani, jijini baada ya kutoka katika vipindi vyao vya masomo. Tunda moja liliuzwa kati ya sh 50 na 100 kutegemea ukubwa.

Tuesday, April 13, 2010

WAZEE WA AFRIKA MASHARIKI WADUNDA KWA KOVA, AWAMWAGIA AYA ZA QUR'AN...

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman kova leo amewasihi wazee wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutopenda kujihusisha na vurugu ambazo mwisho wake hupelekea jeshi lake kutumia nguvu za dola sheria dhidi yao.

Kamishna Kova amesema kuwa kwa mujibu wa desturi za kiafrika, unapompiga mzee huenda ukapata lana kutoka kwa mungu na hivyo si jambo jema kwake kuwachukulia hatua za kipolisi ambazo mwisho wake huwa ni maumivu.

'Mimi naogopa laana wazee wangu. Sipendi mimi kuona mnachukuliwa nguvu za kisheria dhidi yenu." Aliwasihi na kuendelea, "Kwa wale wanaoamini kitabu cha Qur'an kinasema kuwa Innallaah maa swaabirina... Maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu yupo karibu na mwenye subira.. hivyo bawasihi mfanye subira hili jambo lenu nitalishughulikia mimi pamoja na hawa viongozi wenu", Alimaliziia kwa kusema hivyo na kuwafanya wazee hao waliokuwa wamekusanyika mbele ya Kituo Kikuu cha Polisi 'Central Police' kumshangilia kwa makofi...

Kisha akawasihi wazee hao kwa kuwaambia tena, "Hivyo nawaomba wazee wangu muende nyumbani kwa amani... hili suala niachieni mimi na viongozi wenu mliowaamini... sawa jamani?" Alimalizia kwa kusema hivyo na kisha wazee wale baada ya sekunde chache wakaridhia maneno yake na wakaondoka zao...


Wazee wa Afrika Mashariki wakiondoka zao baada ya kumwagiwa aya na Kova...

DK. MNDOLWA MWENYEKITI MPYA WA BODI BENKI YA KCB TANZANIA

Benki ya KCB Tanzania imepata Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ambaye ni Dk. Edmund Mndolwa ambaye ameshika nafasi ya Mhe. Janet Mbene ambaye kwa sasa ni Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kufanyika kwa mabadiliko haya kumezingatia mwongozo wa Benki Kuu ya Tanzania kwa wakurugenzi wa mabenki na taasisi za kifedha wa mwaka 2008 ambao unawazuia wabunge kushika nyadhifa za ukurugenzi wa taasisi za kifedha.



Mwenyekiti mpya wa bodi, Dk. Edmund Mndolwa (kulia) akifafanua jambo

ZAIN WAZINDUA SHILINGI 1 KWA SEKUNDE, USIKU SEKUNDE 60

Kampuni ya simu za mkononi ya Zain leo imezindua huduma ya malipo ya shilingi 1 kwa sekunde. Na kwa usiku ni shilingi 1 kwa sekunde 60. Huduma hiyo inafahamika kwa jina la 'Uhuru wa Kuongea'.

Mkurugenzi Mkuu wa Zain, Khaled Muhtadi amesema hiyo ni katika sehemu ya kuboresha huduma za mtandao huo na kuwapa unafuu wateja wake kuweza kumudu gharama za mtandao huo.

'Hii itakuwa ni huduma ya kwanza kwetu kuweza kuwapa unafuu wateja wetu kuweza kumudu gharama za matumizi." Alisema.


Zain officials display billiboards showing 1 tsh tariff 24 hrs

Tuesday, April 6, 2010

KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA RWANDA KUADHIMISHA KESHO MLIMANI CITY

Maadhimisho ya Kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari, nchini Rwanda yanatarajiwa kufanyika kesho katika Viwanja vya Mlimani City kuanzia saa 9 alasiri.

Balozi wa Rwanda nchini, Fatuma Ndangiza amewaambia waandishi wa habari leo jijini hapa alipofanya nao mkutano.

Balozi Ndangiza amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo.


BALOZI FATUMA NDANGIZA

DOKTA KUMNG'OA LOWASSA JIMBONI

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Dk. Salash Toure ametangaza nia yake ya kugombea Ubunge katika jimbo la Monduli, alipozungumza na waandishi wa habari mjini Arusha leo.

Kwa sasa jimbo hilo linaongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa.


DK TOURE