Monday, November 16, 2009

ANNE KILANGO AMWAGA MACHOZI SAME

Safari ilianza hivi:


Mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela alianza safari yake ya kupanda mlima kuelekea kwenye maafa akisaidiwa na Mbunge wa Vunjo, Alloyce Kimaro (kulia).


Bada ya kushuhudia maafa hayo, Mbunge huyu alishindwa kujizuia na kuanza kuangua kilio hadharani... Lakini wamama wa kijijini pale walimfariji...


Hapa akina mama hawa wa kijijini hapo wakiendelea kumfariji Mama Anna kilango..


Baada ya hapo Mama Anne Kilango alimshukuru Mungu na kumuomba awalaze marehemu wote mahala pema peponi kama anavyoonekana...

Maporomoko ya Miamba yaliyotokea wiki iliyopita katika Kijiji cha Goha, Wilayani Same na kusababisha vifo vya watu 24 mpaka kufikia jana. Pia mali mbalimbali za wanakijiji hao ziliharibika ikiwamo mazao ya shambani, mifugo na kadhalika...

Mungu azilaze roho za Marehemu hao mahala pema peponi.

No comments:

Post a Comment