Sunday, November 22, 2009

ELIMU YA AJABU NDANI YA MSITU

Unaweza ukastaajabu lakini ni kweli... Hili ni tukio la aina yake ambalo wengi wetu tumekuwa tukisikia tu kupitia vyombo mbalimbali vya habari na kadhalika... Katika hali isiyo ya kawaida Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya amewakuta watoto wadogo wakazi wa Kijiji cha Igumbiro, Tarafa ya Lupiro, Wilayani Ulanga zaidi ya kilometa 12 toka kijijini mwishoni mwa wiki wakifundishwa kusoma, kuandika, kuhesabu na kujua lugha ya kiswahili ndani ya Msitu wa hifadhi ya asili wa Nanji.

Watoto hao walikuwa wakifundishwa na mwalimu asiye rasmi aliyetambulika kwa jina la Msuya Shaaban.


Watoto hao wakiwa na mwalimu wao msituni...

No comments:

Post a Comment