Monday, November 2, 2009

JK aipa changamoto Sekta ya Afya

Rais Jakaya Kikwete leo amefungua rasmi shule ya meno ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi za Tiba na Afya Muhimbili (MUHAS, jijini ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali yake ya kuboresha sekta ya Afya kwa nyanja zote.

Mbali na shule hiyo, pia Rais Kikwete alifungua huduma mbalimbali zitakazoanza kutolewa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili zikiwemo matibabu ya figo na nyinginezo.

Rais Kikwete amesema Serikali yake imedhamiria kuboresha afya za wananchi kwa kuhakikisha inatoa fungu kubwa la fedha kugharamia zahanati za vijijini, kata na hospitali za wilaya.

"Afya za wananchi zikiwa bora, na maisha yao yatakuwa bora. Kila mtanzania apate huduma ya afya, tujenge vituo vya afya, zahanati karibu na wananchi." Alisema leo.

Rais Jakaya Kikwete, wadau wa afya na wataalamu mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na mashine ya kupima figo leo mchana Muhimbili

No comments:

Post a Comment