Thursday, April 21, 2011

OPERESHENI YA SHIRIKA LA NYUMBA YAMKUMBA OFISA MSTAAFU WA USALAMA WA TAIFA


Leo majira ya saa nne asubuhi, kwenye mtaa wa Uhuru, nyumba namba 102 ya Shirika la nyumba (NHC), ilikuwa ni siku mbaya kwa familia ya Ofisa Mstaafu wa Usalama wa Taifa, aliyefahamika kwa jina la Aboubakar Kapera baada ya vibarua wa kampuni ya udalali ya Kimbembe kuvamia makazi yake na kuanza kuhamisha vyombo nje kwa ajili ya kuvipiga mnada.

Operesheni hiyo iliyo chini ya NHC, ni ya kukusanya madeni yake kwa wadaiwa sugu ambao wameshindwa kulipa kodi zao kwa muda mrefu.

MPIGANIA UKOMBOZI WA KOSOVO AONDOKA NCHINI KUELEKEA BURUNDI KUENDELEZA KAMPENI YAKE

Kapteni James Bareshi, ambaye ni raia wa jimbo la Kosovo lililo chini ya utawala wa Urusi ameondoka leo nchini kuelekea Burundi kuendeleza harakati zake za kampeni ya kutaka jimbo hilo kuwa nchi inayojitawala yenyewe.

James, ambaye anatumia ndege ndogo ya abiria watatu yenye ujumbe unaosomeka "PLEASE RECOGNIZE THE INDEPENDENCE OF KOSOVO" anatembelea nchi mbalimbali duniani kusambaza ujumbe wake huo. Juzi James, alikuwa hapa nchini ambapo alikutana na vyombo mbalimbali vya habari akizungumzia azma yake hiyo ya kutaka Kosovo kuwa nchi huru.



Kwa mujibu wa msaidizi wake ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema kuwa, James hutua ardhini kila baada ya saa nne kwa ajili ya kuongeza mafuta kwenye ndege yake ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na safari inazokwenda.

James, ambaye ni 'PILOT' kitaaluma, anapata ufadhili wa raia wa Kosovo wanaoishi maeneo mbalimbali ya dunia kwa kufanya harambee kwa ajili ya kuhakikisha anafanikisha zoezi lake hilo.



Ndege ndogo anayotumia James Bareshi kusafiria

TTCL WATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MILIPUKO GONGO LA MBOTO

Kampuni ya simu ya TTCL leo imekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama kwa niaba ya waathirika wa milipuko ya mabomu, Gongo la Mboto leo.

Lakini kwa mtazamo wangu, hawa wanaotoa misaada kwa waathirika wa milipuko ya mabomu Gongo la Mboto ni vema sasa wakabadilisha aina ya misaada na badala yake wakaenda kuona ni kwa kiasi gani wanavyoathiriwa na mvua za Masika zinazoendelea kunyesha hapa jijini.

Naamini, wengi wao bado wanaendelea kulala kwenye mahema, ambayo kwa kiasi kikubwa hayawezi kuhimili mikiki mikiki ya mvua hizi kwa sasa. Wengi wa waathirika hao, ni wale wenye familia wakiwemo watoto wadogo ambao naamini kwa kiasi kikubwa ndiyo waathirika wa mvua hizi.

Hivyo licha ya wahisani kuendelea kuonyesha moyo wa upendo kwa kutoa misaada, ni vema sasa wakaangalia upande wa pili hasa msimu huu wa mvua za masika.



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama akikabidhiwa msaada wa vyakula na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya simu nchini TTCL, Said Amir Said

DK SHEIN AKUTANA NA BALOZI DIANNE CORNER WA UINGEREZA IKULU ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohammed Shein akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianne Corner, Ikulu Zanzibar leo

Pics/source: Ikulu, Zanzibar

SALMA KIKWETE ATEMBELEA THUNDERBIRD SCHOOL OF GLOBAL MANAGEMENT, ARIZONA, MAREKANI

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Salma Kikwete yupo nchini Marekani akiendelea na ziara yake kwenye majimbo mbalimbali ya nchi hiyo. Leo Mama Salma alitembelea shule ya Thunderbird pamoja na kuzungumza na wanafunzi wa shule hiyo.


Salma Kikwete akizungumza na kujibu maswali mbalimbali ya wanafunzi wa shule hiyo (hawapo pichani)


Salma Kikwete akiongozwa na Mwenyeji wake, ambaye ni Rais wa shule hiyo, Dk Angel Cabrera kuangalia eneo la shule hiyo

Pics/Source: Mwanakombo Jumaa, Maelezo

Monday, April 18, 2011

ZA MWIZI AROBAINI



Wakazi wa Buza Cape Town, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam wakiangalia mwili wa kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Iddi ambaye ni mkazi wa Buza Kinyantira aliyeuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za wizi.

Kijana huyo anadaiwa kufumwa akiiba kuku katika moja ya banda la kuku huko Buza, ambapo wananchi hao walianza kukumponda kwa mawe na vitu vizito mpaka kupelekea kifo chake.

Hata hivyo baadaye, askari polisi waliuchukua mwili wake na kwenda kuuhifadhi kwenye chumba cha Maiti cha hospitali ya Temeke jijini, ambapo ndugu zake walikuja kuuchukua kwa mazishi.

PIC/SOURCE: Inno

MARAIS AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA KUJADILI UCHUMI WA AFRIKA

Marais watano wa nchi za Afrika Mashariki leo wamekutana kwa mara ya tisa kujadili maendeleo ya ukuaji wa uchumi kwa nchi zao, kwenye ukumbi wa mikutano Mlimani City, jijini Dar es Salaam leo.

Mkutano huo wa tisa wa uwekezaji barani Afrika umewakutanisha marais, Jakaya Kikwete wa Tanzania, Pierre Nkurunzinza wa Burundi, Mwai Kibaki wa Kenya, Yoweri Museveni wa Uganda, Dk Ali Mohamed Shein wa Zanzibar na Waziri Mkuu wa Rwanda, Bernard Mukuza.



Marais hao wakiwa kwenye mkutano huo

ZANZIBAR SASA KUPATIWA UMEME WA UHAKIKA UTAKAOPITA CHINI YA BAHARI

Akunti ya Mfuko wa Millennium Challenge Tanzania (MCA-T), leo imetiliana saini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa mradi wa umeme kwa mji wa Zanzibar na Kampuni ya umeme ya India Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, jijini Dar es Salaam.

Mkataba huo uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 9 za kitanzania utasaidia ujenzi wa mradi huo utakaoanzia kwenye Kituo cha Ubungo mpaka Ras Kiromoni kwa bara ambapo utapita chini ya bahari na kuibukia Ras Fumba huko Zanzibar kabla ya kuishia kwenye kituo cha Mtoni mjini humo, ukiwa na urefu wa Kilomita 42.



Ofisa Mtendaji Mkuu wa MCA-T, Bernard Mchomvu (kushoto) akibadilishana hati za mkataba huo na Makamu wa Rais wa Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, Vilas Hiremani

DK BILAL ASAINI KITABU CHA RAMBIRAMBI YA MAKAMU WA RAIS WA ZAMANI WA BRAZIL

Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal leo ameweka saini kitabu cha rambirambi ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa zamani wa Brazil, Jose Alencar da Silva kwenye ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo, leo jijini Dar es Salaam.



Dk Bilal akisaini kitabu cha rambirambi

MAOFISA WA POLISI NA ELIMU YA KUPAMBAA NA UHALIFU

Programu ya mafunzo ya siku tatu kwa wakuu wa polisi na wilaya nchini katika kubaini, kuzuia na kudhibiti uhalifu kupitia mfumo wa ulinzi ushirikishi imefunguliwa jana mjini Dodoma na kushirikisha maofisa hao kutoka maeneo mbalimbali ya nchi



Baadhi ya maofisa hao wakifuatilia sehemu ya mafunzo hayo

KONGAMANO LA KUPAMBANA NA KUGHUSHI NYARAKA MWEZI UJAO

Kongamano la elimu ya kupambana na ughushi mbalimbali wa nyaraka na fedha haramu kupitia mtandao linatarajiwa kufanyika jijini hapa mwezi ujao.


Mwakilishi wa asasi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na upambanaji wa matukio hayo nchini, Solomon Njiamoja akifafanua jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari leo. Mwingine ni Mkurugenzi wa kampuni ya D'Sullivan ya Nairobi, Kenya, Sosthenes Bichang'a.

Friday, April 15, 2011

BATA LA MARIPOTA WA KILI TAIFA CUP SOUTH BEACH LEO

WAANDISHI wa habari za michezo, hususan wa mashindano ya Kili Taifa Cup, leo walikuwa na wakati mzuri ambapo walifanyiwa semina na kisha kushiriki michezo, kula na kunywa, kwenye hoteli ya South Beach, Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Michezo waliyoshiriki ni pamoja na soka kwa mashabiki wa timu mbili mashuhuri za Simba na Yanga ambapo mwisho wa mchezo Yanga waliibuka kidedea kwa kushinda bao moja.

Yafuatayo ni matukio ya bata hilo kwenye picha


Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, David Minja akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Simba, .Amri Massare


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Yanga, Muhidin Sufiani


Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akijibu maswali ya waandishi hao


Waandishi w ahabari za michuano ya Kili Taifa Cup inayotarajiwa kuanza mwezi ujao wakipata darasa