Monday, April 18, 2011

ZANZIBAR SASA KUPATIWA UMEME WA UHAKIKA UTAKAOPITA CHINI YA BAHARI

Akunti ya Mfuko wa Millennium Challenge Tanzania (MCA-T), leo imetiliana saini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa mradi wa umeme kwa mji wa Zanzibar na Kampuni ya umeme ya India Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, jijini Dar es Salaam.

Mkataba huo uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 9 za kitanzania utasaidia ujenzi wa mradi huo utakaoanzia kwenye Kituo cha Ubungo mpaka Ras Kiromoni kwa bara ambapo utapita chini ya bahari na kuibukia Ras Fumba huko Zanzibar kabla ya kuishia kwenye kituo cha Mtoni mjini humo, ukiwa na urefu wa Kilomita 42.



Ofisa Mtendaji Mkuu wa MCA-T, Bernard Mchomvu (kushoto) akibadilishana hati za mkataba huo na Makamu wa Rais wa Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, Vilas Hiremani

No comments:

Post a Comment