Thursday, April 21, 2011

OPERESHENI YA SHIRIKA LA NYUMBA YAMKUMBA OFISA MSTAAFU WA USALAMA WA TAIFA


Leo majira ya saa nne asubuhi, kwenye mtaa wa Uhuru, nyumba namba 102 ya Shirika la nyumba (NHC), ilikuwa ni siku mbaya kwa familia ya Ofisa Mstaafu wa Usalama wa Taifa, aliyefahamika kwa jina la Aboubakar Kapera baada ya vibarua wa kampuni ya udalali ya Kimbembe kuvamia makazi yake na kuanza kuhamisha vyombo nje kwa ajili ya kuvipiga mnada.

Operesheni hiyo iliyo chini ya NHC, ni ya kukusanya madeni yake kwa wadaiwa sugu ambao wameshindwa kulipa kodi zao kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment