Monday, April 18, 2011

ZA MWIZI AROBAINI



Wakazi wa Buza Cape Town, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam wakiangalia mwili wa kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Iddi ambaye ni mkazi wa Buza Kinyantira aliyeuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za wizi.

Kijana huyo anadaiwa kufumwa akiiba kuku katika moja ya banda la kuku huko Buza, ambapo wananchi hao walianza kukumponda kwa mawe na vitu vizito mpaka kupelekea kifo chake.

Hata hivyo baadaye, askari polisi waliuchukua mwili wake na kwenda kuuhifadhi kwenye chumba cha Maiti cha hospitali ya Temeke jijini, ambapo ndugu zake walikuja kuuchukua kwa mazishi.

PIC/SOURCE: Inno

No comments:

Post a Comment