Thursday, April 21, 2011

MPIGANIA UKOMBOZI WA KOSOVO AONDOKA NCHINI KUELEKEA BURUNDI KUENDELEZA KAMPENI YAKE

Kapteni James Bareshi, ambaye ni raia wa jimbo la Kosovo lililo chini ya utawala wa Urusi ameondoka leo nchini kuelekea Burundi kuendeleza harakati zake za kampeni ya kutaka jimbo hilo kuwa nchi inayojitawala yenyewe.

James, ambaye anatumia ndege ndogo ya abiria watatu yenye ujumbe unaosomeka "PLEASE RECOGNIZE THE INDEPENDENCE OF KOSOVO" anatembelea nchi mbalimbali duniani kusambaza ujumbe wake huo. Juzi James, alikuwa hapa nchini ambapo alikutana na vyombo mbalimbali vya habari akizungumzia azma yake hiyo ya kutaka Kosovo kuwa nchi huru.



Kwa mujibu wa msaidizi wake ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema kuwa, James hutua ardhini kila baada ya saa nne kwa ajili ya kuongeza mafuta kwenye ndege yake ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na safari inazokwenda.

James, ambaye ni 'PILOT' kitaaluma, anapata ufadhili wa raia wa Kosovo wanaoishi maeneo mbalimbali ya dunia kwa kufanya harambee kwa ajili ya kuhakikisha anafanikisha zoezi lake hilo.



Ndege ndogo anayotumia James Bareshi kusafiria

No comments:

Post a Comment