Friday, April 15, 2011

BATA LA MARIPOTA WA KILI TAIFA CUP SOUTH BEACH LEO

WAANDISHI wa habari za michezo, hususan wa mashindano ya Kili Taifa Cup, leo walikuwa na wakati mzuri ambapo walifanyiwa semina na kisha kushiriki michezo, kula na kunywa, kwenye hoteli ya South Beach, Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Michezo waliyoshiriki ni pamoja na soka kwa mashabiki wa timu mbili mashuhuri za Simba na Yanga ambapo mwisho wa mchezo Yanga waliibuka kidedea kwa kushinda bao moja.

Yafuatayo ni matukio ya bata hilo kwenye picha


Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, David Minja akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Simba, .Amri Massare


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Yanga, Muhidin Sufiani


Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akijibu maswali ya waandishi hao


Waandishi w ahabari za michuano ya Kili Taifa Cup inayotarajiwa kuanza mwezi ujao wakipata darasa

No comments:

Post a Comment