Thursday, April 21, 2011

TTCL WATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MILIPUKO GONGO LA MBOTO

Kampuni ya simu ya TTCL leo imekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama kwa niaba ya waathirika wa milipuko ya mabomu, Gongo la Mboto leo.

Lakini kwa mtazamo wangu, hawa wanaotoa misaada kwa waathirika wa milipuko ya mabomu Gongo la Mboto ni vema sasa wakabadilisha aina ya misaada na badala yake wakaenda kuona ni kwa kiasi gani wanavyoathiriwa na mvua za Masika zinazoendelea kunyesha hapa jijini.

Naamini, wengi wao bado wanaendelea kulala kwenye mahema, ambayo kwa kiasi kikubwa hayawezi kuhimili mikiki mikiki ya mvua hizi kwa sasa. Wengi wa waathirika hao, ni wale wenye familia wakiwemo watoto wadogo ambao naamini kwa kiasi kikubwa ndiyo waathirika wa mvua hizi.

Hivyo licha ya wahisani kuendelea kuonyesha moyo wa upendo kwa kutoa misaada, ni vema sasa wakaangalia upande wa pili hasa msimu huu wa mvua za masika.



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama akikabidhiwa msaada wa vyakula na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya simu nchini TTCL, Said Amir Said

No comments:

Post a Comment