Sunday, August 30, 2009

ARE WE SAFE?

Hii ni chemchem ya maji machafu inayotiririkia katika bahari ya Hindi, eneo la Ufukwe wa Gymkhana, Dar es Salaam. Eneo hili lina umuhimu sana kwa watoto na hata wakubwa kwa kuja kujipumzisha siku za mwisho wa wiki.

Wakati mwingine watoto hawa na wakubwa huogelea kwa ajili ya kupunguza joto la jiji hapa. Lakini hatari iliyopo na ambayo huenda tayari imeshajitokeza kwa watoto hawa na wakubwa, ni magonjwa ya kuambukizwa, mfano ngozi, homa za matumbo na kadhalika.

Hii inatokana na kiasi kikubwa cha maji wanayotumia kwa kuoga kuathiriwa na majitaka kama si ya 'kinyesi' yanayotirikia katika ufukwe huo. Haiyumkini maji haya yanatoka wapi, lakini harufu yake kali inatosha ku'define' kuwa maji haya si salama hata kwa kuvuta harufu yake.

Sihitaji kuuliza kama Mamlaka husika imeliona hili ama la, lakini wajibu wangu kama mpashaji wa habari na matukio nachukua fursa hii kuzihoji Mamlaka ya Majisafi na Majitaka jijini hapa (DAWASA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji, (Dar es Salaam City Council) kama wanalifahamu hili ama la, na kama wanalifahamu kuna hatua gani zinachukuliwa kunusuru hali hii?


"Haya ndiyo majitaka yanayoingia baharini..." ni kama anaonesha ishara ya kusema hivi huyu mkazi...

No comments:

Post a Comment