Friday, August 7, 2009

JIJI, USALAMA WA AFYA ZETU UNAZINGATIWA?

Hali ya usafi katika soko la samaki Magogoni (Ferry) si ya kuridhisha. Hii imekuwa ni hali sugu sasa kutokana na kutofanyiwa kazi kama si kumalizwa kabisa kwa tatizo hili, sokoni hapo.

Si jambo la kustaajabisha kushuhudia mitaro ya maji machafu yenye harufu kali ikitiririkia baharini wakati mvuvi akiwaosha samaki wake katika maji hayo kabla ya kupeleka kwa wanunuzi..

Lakini hili lisionekane kama ni tatizo la kawaida kwa maana mimi na wewe ambao tunakifurahia kitoweo cha samaki wa baharini hasa wale wanaotoka sokoni hapo hatujui mpaka sasa usalama wa afya zetu ukoje?

Halmashauri ya Jiji kwa kushirikiana na Mamlaka husika inayosimamia shughuli za uendeshaji wa soko hilo hauna budi kuliangalia hili kwa macho mawili, vinginevyo afya zetu haziko salama hata kidogo...



Mchuuzi akipita kwa shida katika mitiririko ya maji machafu yenye harufu kali, inayoingia baharini eneo la uvuvi...


Hali si nzuri.. Angalia mchuuzi huyu wa samaki akipita katika michuruziko hii ya maji machafu yenye harufu kali inayoingia baharini, eneo la soko la samaki...

No comments:

Post a Comment