Thursday, August 6, 2009

Mkenya mwanamama anaswa Ubungo stendi na dawa za kulevya..

Amini usiamini... Mama mmoja raia wa Kenya, aliyefahamika Kwa jina la REBECCA WAIRIMU amenaswa na UNGA wa dawa za kulevya aina ya HEROIN pale Ubungo Bus Terminal, jana jioni na mashushu wa kibongo...

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya, ACP Godfrey Nzowa, mama huyo alikuwa akitokea Kenya kwenda SOUTH AFRICA kwa mzee ZUMA huko kwa ajili ya kutafuta soko la dawa hizo..

Mara baada ya kushuka stendi ya ubungo jana jioni, mashushu wakamtilia mashaka na kuanza kumpekua... ndipo walipomkuta na dawa hizo. unga huo unakadiriwa kuwa na uzito wa kilo 3 na thamani yake bado haijajulikana...

Kwa sasa mama huyo anashikiliwa na mashushu hao... na mara baada ya uchunguzi kukamilika kama atabainika na makosa basi atafunguliwa mashtaka...


Na hivi ndivyo mama huyo alivyoficha hayo madawa ya kulevya aina ya Heroin... Hapa Mkuu wa kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya nchini, ACP Godfrey Nzowa akizitafuta dawa hizo baada ya kubaini... Anaanza kwa kutoa nguo zilizomo ndani ya begi..


kisha nguo zote zimekwisha.. sasa 'unga' uko wapi?... hebu angalia sasa picha ya chini uone namna mwanamama huyo alivyokuwa ameuficha UNGA huo kwa chini kwabisa ili usigundulike...


Amini usiamini... huu ni mfuko ambao umenakshiwa kwa kahawa na ndani yake sasa ndio kuna unga wa dawa za kulevya aina ya HEROIN...


Hii ni pasipoti yake ya kusafiria...

No comments:

Post a Comment