Sunday, August 30, 2009

BOMU JINGINE LALIPUKA MBAGALA

WAKATI waathirika wa mabomu yaliyotokea eneo la Mbagala Kuu karibu na kambi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakiendelea kulipwa fidia zao juzi kulitokea mlipuko na kusababisha baadhi ya wakazi hao kukimbia.

Mlipuko huo ulitokea juzi saa 1:30 usiku mtaa wa Mbagala Kuu baada ya msimamizi wa nyumba hiyo Elisi Emmanuel kukusanya uchafu na kuchoma takataka kwenye nyumba yenye namba MA/1/2835 na kujiandaa na ujenzi upya.

Emmanuel ambaye hakumtaja mmiliki wa nyumba hiyo alisema alikuwa anafanya usafi saa 11:00 jioni na baada ya kufanya usafi huo aliondoka kwa muda lakini ulipofika saa ilipofika saa 1:30 usiku ghafla kulisikika mlio mkubwa hali iliyopelekea waathirika ambao walikuwa mamemaliza kufturu kutokana na mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan kukimbia ili kujinusuru na maisha yao.

**Veronica Mheta**

No comments:

Post a Comment