Thursday, March 25, 2010

CHINA YAMWAGA PIKIPIKI 100 DAR CITY



Halmashauri ya Jiji la Changzho, China imetoa msaada wa pikipiki 100 kwa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kusaidia maendeleo katika kata zake.

Meya wa jiji hilo Weng Wengcheng amesema msaada huo ni matunda ya ushirikiano mzuri baina ya nchi hizo mbili hususan miji hii miwili ya Changzhou na Dar es Salaam.

Miji hiyo ni miji dada kutokana na ushirikiano wa kiuchumi uliopo kati yao.

No comments:

Post a Comment