Monday, March 22, 2010

UANDIKISHAJI WAPIGAKURA WAANZA LEO DAR



Zoezi la kuboresha daftari la wapigakura limeanza leo katika vituo mbalimbali vilivyoteuliwa, jijini hapa leo.

Sponsor ilishuhudia maeneo mbalimbali hasa katika shule za msingi kukiwa na mikusanyiko ya wananchi wakijiandikisha katika daftari la wapigakura.

Vituo hivyo ni Hananasif Kinondoni, Basata Ilala na Shule ya Msingi Makamba Temeke.

"Kwa ujumla zoezi limeanza vizuri, wananchi wameitikia wito." Alisema Flora Luhamo, mwandikishaji wa kituo cha Hananasif.

No comments:

Post a Comment