Rais Kikwete amemwapisha ndugu Dk. Phillip Isidori Mpango kuwa Katibu Mtendaji wa Tue ya Mipango, Bw. Maduka Paul Kessy kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa tume hiyo pamoja na Bi. Happiness Ngoti Mgalula naye pia kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa tume hiyo.

Wengine ni Bi. Florence Mwanri ambaye ni Naibu Katibu wa Tume hiyo ya Mipango na Bw. Clifford Katondo Tandali naye pia kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo.
Hafla ya kuwaapisha Katibu na Manaibu Katibu wake imefanyika Ikulu, jijini Dar es Salam leo asubuhi.
No comments:
Post a Comment