Friday, March 5, 2010

MUHIMBILI SACCOS YAMWAGA VYANDARUA KWA WAGONJWA

Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) kwa wafanyakazi wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili leo kimetoa msaada wa vyandarua 100 vyenye thamani ya sh 580,000/ kwa Mama na Watoto katika hospitali ya Muhimbili.

Msaada huo umekuja siku chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza Kampeni ya Zinduka, inayopiga Vita Ugonjwa wa Malaria.


Mwenyekiti wa SACCOS hiyo (kushoto) akikabidhi vyandarua hivyo

No comments:

Post a Comment