Wednesday, October 28, 2009

BOMU LAUA 90 PAKISTAN

Bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari limelipuka na kuua watu 90, eneo la sokoni, Pashawar, nchini Pakistani leo idadi kubwa ikiwa ni wanawake, serikali imesema.

Mlipuko huo ambao umetokea katika Bazaar ya Meena umejeruhi zaidi ya watu 200, kwa mujibu wa Waziri wa Habari wa Jimbo la kaskazini Magharibi.

Inasemekana mlipuko huo utakuwa ni miongoni mwa milipuko mikubwa zaidi kutokea katika jimbo hilo likihusisha vifo zaidi vya kina mama.

No comments:

Post a Comment