Saturday, October 3, 2009

SIMBA HAIKAMATIKI, YANGA YAJISOGEZA...

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, klabu ya soka ya Yanga leo imefuta uteja wa kurambishwa sukari na timu ya Kagera Sugar baada ya kuichapa kwa magoli 2-0katika mechi iliyochezwa uwanja wa Kaitaba, Bukoba leo, wakati Simba ya Dar es Salaam ambayo inaongoza Ligi ikishinda dhidi ya Moro United kwa magoli 2-1.


Mlinda mlango wa timu ya Moro United, Rajab Masud pamoja na Nahodha wake Wazir Mahadhi wakiangalia mpira ukiingia wavuni kuandika goli la kwanza, huku mshambuliaji wa Simba, Mussa Hassan Mgosi akijiandaa kwa lolote litakaloweza kutokea wakati wa michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, iliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam leo

1 comment:

  1. hello... hapi blogging... have a nice day! just visiting here....

    ReplyDelete