Saturday, October 3, 2009

MISS TANZANIA: BADO KUNA TATIZO

Mrembo wa Tanzania 2009 Miriam Gerald amepatikana katika kinyang'anyiro kilichofanyika usiku wa kuamkia leo, jijini hapa Dar es Salaam. Tunaishukuru kamati ya Miss Tanzania ikiongozwa na Hashim Lundenga 'Uncle' kwa kufanikisha hilo, na kuwa na moyo wa kujitolea tangu mbio hizo zilipoanza.

Pongezi hizo ziende sambamba na changamoto katika kamati hii ya Miss Tanzania, ambayo ni tatizo la kujieleza kwa washiriki wetu pindi inapofikia hatua ya maswali. Jana tulishuhudia baadhi ya warembo hao wakishindwa kujieleza vizuri mbele ya hadhira jambo lililopelekea wengine kutoa majibu yasiyoeleweka.

Nampongeza sana Miriam, ambaye ndiye Miss Tanzania 2009, kwa kujieleza vema kwa usahihi hasa alipoamua kutumia lugha ya kiswahili ambayo ndiyo ya Taifa, ambo lililompa uhuru wa kujieleza na kueleweka kwa majaji, na washabiki waliokuwa wamehudhuria mashindano hayo.

Mungu ibariki lugha yetu ya Kiswahuili, Mungu ibariki Tanzania!


Vodacom Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Beatrice Lukindo (kulia) na mshindi wa tatu Sia Ndasikoi, baada ya kutangzwa washindi wa shindano hilo Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo

No comments:

Post a Comment