Tuesday, October 27, 2009

Tigo yakabidhi vifaa vya michezo

Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo leo imekabidhi vifaa vya michezo kwa wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi ili kuiwezesha timu yake kufanya vema katika mashindano ya SHIMIWI yanayoendelea mjini Morogoro.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya shs milioni 6.8 ni pamoja na viatu vya mpira seti 2, jezi za netball 14, track suits jozi 44, jezi za mchezo wa riadha jozi 6, mipira ya miguu 10 na mipira ya pete 5.


Ofisa uhusiano wa Tigo, Jackson Mmbando (kulia) akikabidhi vifaa hivyo kwa Kamishna Uhamiaji anayeshughulikia Sheria, Wizara ya Uhamiaji na Mambo ya Ndani, Magnus Ulingi

No comments:

Post a Comment