Friday, August 13, 2010

CHATU WA KEKO APATIKANA



Chatu aina ya Sebei au 'African Rock Python' mwenye uzito wa kilogramu 8, urefu wa futi 7 na umri wa miaka 6, aliyekuwa amepotea siku kumi zilizopita Wizara ya Maliasili na Utalii, amepatikana leo.

Chatu huyo ambaye alizua hofu kubwa miongoni mwa wakazi wanaoishi kata ya Keko, jirani na wizarani hapo, alipatikana majira ya saa 6.30 mchana wa leo akiwa amejificha kwenye mazulia mabovu na majenereta, ndani ya eneo hilo la wizara.

Kwa mujibu wa watumishi wa wizarani hapo, chatu huyo alikuwa akikamata panya na kula kwa siku hizo kumi. Lakini pia wamesema hakuna madhara yoyote yaliyotokea.

CHATU PICHANI:



No comments:

Post a Comment