Monday, August 9, 2010

HAPA NDIPO ANAPOANDALIWA PWEZA?



Mkazi huyu wa jijini Dar es Salaam alikutwa na blogu hii akiandaa samaki aina ya pweza na ngisi kwenye mazingira machafu leo asubuhi, Soko la Samaki Magogoni (Feri). Maandalizi ya chakula kwenye mazingira ya aina hii ni hatari hasa ukuzingatia mtumiaji ni binadamu mimi na wewe.

Mamlaka zinazohusika na masuala ya usafi wa mazingira kwenye maeneo nyeti hasa Sokoni hazina budi kuchukua tahadhari kwa kufanya ziara za mara kwa mara maeneo hayo kuhakikisha wafanyabiashara wanafuata taratibu na kanuni za usafi wakati wakiandaa bidhaa zao ili kuepusha maradhi ya milipuko kwa watumiaji.

No comments:

Post a Comment