Vituko vilianza kuibuka kwenye matawi mbalimbali huku kukiwa na malalamiko kadhaa kwa wanachama kuzuiliwa kupiga kura kutokana na majina yao kutoorodheshwa kwenye rejista mpya. Tawi la Misewe, Darajani na Segerea yote yakiwa kwenye Jimbo la Segerea malalamiko yalikuwa ya aina hiyo.

Jangwani, vituko vya kubiduliwa biduliwa kwa masanduku ya kupigia kura vilileta sura tofauti kabisa. Sababu inadaiwa ni kuwa majina ya watu yalikutwa yamepewa tiki kwenye rejesta ya majina.
Halikadhalika, kwenye Tawi moja lililopo Magomeni, zaidi ya kadi 500 za CCM zilirudishwa na wanachama wake na kuchukua za CUF papo hapo kutokana na kutoridhishwa na mchakato mzima wa zoezi hilo.
Tutaendelea kuwaletea updates za matokeo... Endelea kuhabarika
No comments:
Post a Comment