Monday, August 1, 2011

LAGHAI MZOEFU ANASWA MTAA WA KONGO

Usithubutu kusimamisha gari lako pindi akufuatapo na kuanza kukwambia umemgonga! Kitakachofuatia ni kukupora kila kitu kilichomo kwenye gari lako. Huyu ni laghai mzoefu aliyekuwa amefumbiwa macho na wafanyabiashara wa Mtaa wa Kongo jijini Dar es Salaam aliyefahamika kwa jina moja la Nurdin. Lakini waswahili wanasema za mwizi arobaini. Leo amenaswa kweupeee na mgambo wa jiji akitaka kumlaghai dereva wa teksi mtaani hapohapo! Fuatilia tukio zima katia 'series' ya picha


Ilianza hivi... Hawa ni Mgambo wa jiji wapo kwenye Patrol yao...


Ghafla wanamkuta 'Nurdin' akiwa amemzuia dereva wa teksi akidai kagongwa...


Mgambo wanashuka ili kujua nini kinachoendelea...


Mgambo baada ya kuhoji na kuambiwa 'Nurdin' ni laghai na ndio staili zake, wanamkwida na kuondoka naye...


Wanamdhibiti kisawasawa ili kumpandisha kwenye gari lao...


'Nurdin' anapingana nao na kuanza kuleta kashkash...


Lakini nguvu ya 'Teja Nurdin' ni ya kitoto sana kwa mgambo hawa... wanampandisha sasa kwenye gari lao...


Hapa amedhibitiwa kisawasawa akiwa ndani ya gari la mgambo hawa...


Hebu 'cheki' sura hii ukiambiwa ni kibaka na tapeli mzoefu utakataa? Mgambo haoooo wanaondoka na Nurdin...

FOLENI BADO YAWATESA WAKAZI DAR


Magari yakiwayamesongamana kwenye Mtaa maarufu wa Samora katikati ya jiji la Dar es Salaam kama ilivyonaswa na kamera ya sponsor leo mchana. Foleni ya magari bado ni kero inayowatesa wakazi wa jiji hilo.

FIFA YAENDESHA MAFUNZO KWA MAKOCHA WANAWAKE


Mkufunzi wa mafunzo ya ukocha kwa wanawake wa FIFA kutoka nchini Namibia, Jacqueline Chipanga akielekeza jambo kwa makocha hao kutoka mikoa mbalimbali nchini wakati wa mafunzo hayo yaliyoanza leo kwenye hoteli ya Rainbow, jijini Dar es Salaam.

WASHINDI TIGO JIPANGE KIMAISHA WAKABIDHIWA MILIONI 5


Washindi wa promosheni ya Jipange Kimaisha inayoendeshwa na kampuni ya simu ya Tigo (kutoka kushoto) Festo Saluni, Jane Mtenga na Nasoro Muharam wakiwa wameshikilia hundi yao ya shilingi milioni 5 mara baada ya kukabidhiwa leo jijini Dar es Salaam.

KOICA YANOGESHA NANENANE MOROGORO


Balozi wa Korea Kusini nchini, Kim Young- Boon (kushoto) akiwa amebeba mgongoni kifaa inachoitwa ‘Jige’ ambacho hutumiwa na wananchi hasa wakulima vijijini nchini Korea Kusini kwa urahisi mara baada ya kufungua Banda la Koica leo mjini Morogoro kwenye Maonesho ya wakulima yaliyoanza kwenye viwanja vya Nanenane mjini humo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Kanali Mstaafu Issa Machibya.
Picha: John Nditi

Thursday, April 21, 2011

OPERESHENI YA SHIRIKA LA NYUMBA YAMKUMBA OFISA MSTAAFU WA USALAMA WA TAIFA


Leo majira ya saa nne asubuhi, kwenye mtaa wa Uhuru, nyumba namba 102 ya Shirika la nyumba (NHC), ilikuwa ni siku mbaya kwa familia ya Ofisa Mstaafu wa Usalama wa Taifa, aliyefahamika kwa jina la Aboubakar Kapera baada ya vibarua wa kampuni ya udalali ya Kimbembe kuvamia makazi yake na kuanza kuhamisha vyombo nje kwa ajili ya kuvipiga mnada.

Operesheni hiyo iliyo chini ya NHC, ni ya kukusanya madeni yake kwa wadaiwa sugu ambao wameshindwa kulipa kodi zao kwa muda mrefu.

MPIGANIA UKOMBOZI WA KOSOVO AONDOKA NCHINI KUELEKEA BURUNDI KUENDELEZA KAMPENI YAKE

Kapteni James Bareshi, ambaye ni raia wa jimbo la Kosovo lililo chini ya utawala wa Urusi ameondoka leo nchini kuelekea Burundi kuendeleza harakati zake za kampeni ya kutaka jimbo hilo kuwa nchi inayojitawala yenyewe.

James, ambaye anatumia ndege ndogo ya abiria watatu yenye ujumbe unaosomeka "PLEASE RECOGNIZE THE INDEPENDENCE OF KOSOVO" anatembelea nchi mbalimbali duniani kusambaza ujumbe wake huo. Juzi James, alikuwa hapa nchini ambapo alikutana na vyombo mbalimbali vya habari akizungumzia azma yake hiyo ya kutaka Kosovo kuwa nchi huru.



Kwa mujibu wa msaidizi wake ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema kuwa, James hutua ardhini kila baada ya saa nne kwa ajili ya kuongeza mafuta kwenye ndege yake ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na safari inazokwenda.

James, ambaye ni 'PILOT' kitaaluma, anapata ufadhili wa raia wa Kosovo wanaoishi maeneo mbalimbali ya dunia kwa kufanya harambee kwa ajili ya kuhakikisha anafanikisha zoezi lake hilo.



Ndege ndogo anayotumia James Bareshi kusafiria

TTCL WATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MILIPUKO GONGO LA MBOTO

Kampuni ya simu ya TTCL leo imekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama kwa niaba ya waathirika wa milipuko ya mabomu, Gongo la Mboto leo.

Lakini kwa mtazamo wangu, hawa wanaotoa misaada kwa waathirika wa milipuko ya mabomu Gongo la Mboto ni vema sasa wakabadilisha aina ya misaada na badala yake wakaenda kuona ni kwa kiasi gani wanavyoathiriwa na mvua za Masika zinazoendelea kunyesha hapa jijini.

Naamini, wengi wao bado wanaendelea kulala kwenye mahema, ambayo kwa kiasi kikubwa hayawezi kuhimili mikiki mikiki ya mvua hizi kwa sasa. Wengi wa waathirika hao, ni wale wenye familia wakiwemo watoto wadogo ambao naamini kwa kiasi kikubwa ndiyo waathirika wa mvua hizi.

Hivyo licha ya wahisani kuendelea kuonyesha moyo wa upendo kwa kutoa misaada, ni vema sasa wakaangalia upande wa pili hasa msimu huu wa mvua za masika.



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Leonidas Gama akikabidhiwa msaada wa vyakula na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya simu nchini TTCL, Said Amir Said

DK SHEIN AKUTANA NA BALOZI DIANNE CORNER WA UINGEREZA IKULU ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohammed Shein akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianne Corner, Ikulu Zanzibar leo

Pics/source: Ikulu, Zanzibar

SALMA KIKWETE ATEMBELEA THUNDERBIRD SCHOOL OF GLOBAL MANAGEMENT, ARIZONA, MAREKANI

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Salma Kikwete yupo nchini Marekani akiendelea na ziara yake kwenye majimbo mbalimbali ya nchi hiyo. Leo Mama Salma alitembelea shule ya Thunderbird pamoja na kuzungumza na wanafunzi wa shule hiyo.


Salma Kikwete akizungumza na kujibu maswali mbalimbali ya wanafunzi wa shule hiyo (hawapo pichani)


Salma Kikwete akiongozwa na Mwenyeji wake, ambaye ni Rais wa shule hiyo, Dk Angel Cabrera kuangalia eneo la shule hiyo

Pics/Source: Mwanakombo Jumaa, Maelezo

Monday, April 18, 2011

ZA MWIZI AROBAINI



Wakazi wa Buza Cape Town, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam wakiangalia mwili wa kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Iddi ambaye ni mkazi wa Buza Kinyantira aliyeuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za wizi.

Kijana huyo anadaiwa kufumwa akiiba kuku katika moja ya banda la kuku huko Buza, ambapo wananchi hao walianza kukumponda kwa mawe na vitu vizito mpaka kupelekea kifo chake.

Hata hivyo baadaye, askari polisi waliuchukua mwili wake na kwenda kuuhifadhi kwenye chumba cha Maiti cha hospitali ya Temeke jijini, ambapo ndugu zake walikuja kuuchukua kwa mazishi.

PIC/SOURCE: Inno

MARAIS AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA KUJADILI UCHUMI WA AFRIKA

Marais watano wa nchi za Afrika Mashariki leo wamekutana kwa mara ya tisa kujadili maendeleo ya ukuaji wa uchumi kwa nchi zao, kwenye ukumbi wa mikutano Mlimani City, jijini Dar es Salaam leo.

Mkutano huo wa tisa wa uwekezaji barani Afrika umewakutanisha marais, Jakaya Kikwete wa Tanzania, Pierre Nkurunzinza wa Burundi, Mwai Kibaki wa Kenya, Yoweri Museveni wa Uganda, Dk Ali Mohamed Shein wa Zanzibar na Waziri Mkuu wa Rwanda, Bernard Mukuza.



Marais hao wakiwa kwenye mkutano huo

ZANZIBAR SASA KUPATIWA UMEME WA UHAKIKA UTAKAOPITA CHINI YA BAHARI

Akunti ya Mfuko wa Millennium Challenge Tanzania (MCA-T), leo imetiliana saini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa mradi wa umeme kwa mji wa Zanzibar na Kampuni ya umeme ya India Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, jijini Dar es Salaam.

Mkataba huo uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 9 za kitanzania utasaidia ujenzi wa mradi huo utakaoanzia kwenye Kituo cha Ubungo mpaka Ras Kiromoni kwa bara ambapo utapita chini ya bahari na kuibukia Ras Fumba huko Zanzibar kabla ya kuishia kwenye kituo cha Mtoni mjini humo, ukiwa na urefu wa Kilomita 42.



Ofisa Mtendaji Mkuu wa MCA-T, Bernard Mchomvu (kushoto) akibadilishana hati za mkataba huo na Makamu wa Rais wa Kalpa-Taru Power Transmission Ltd, Vilas Hiremani

DK BILAL ASAINI KITABU CHA RAMBIRAMBI YA MAKAMU WA RAIS WA ZAMANI WA BRAZIL

Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal leo ameweka saini kitabu cha rambirambi ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa zamani wa Brazil, Jose Alencar da Silva kwenye ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo, leo jijini Dar es Salaam.



Dk Bilal akisaini kitabu cha rambirambi

MAOFISA WA POLISI NA ELIMU YA KUPAMBAA NA UHALIFU

Programu ya mafunzo ya siku tatu kwa wakuu wa polisi na wilaya nchini katika kubaini, kuzuia na kudhibiti uhalifu kupitia mfumo wa ulinzi ushirikishi imefunguliwa jana mjini Dodoma na kushirikisha maofisa hao kutoka maeneo mbalimbali ya nchi



Baadhi ya maofisa hao wakifuatilia sehemu ya mafunzo hayo

KONGAMANO LA KUPAMBANA NA KUGHUSHI NYARAKA MWEZI UJAO

Kongamano la elimu ya kupambana na ughushi mbalimbali wa nyaraka na fedha haramu kupitia mtandao linatarajiwa kufanyika jijini hapa mwezi ujao.


Mwakilishi wa asasi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na upambanaji wa matukio hayo nchini, Solomon Njiamoja akifafanua jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari leo. Mwingine ni Mkurugenzi wa kampuni ya D'Sullivan ya Nairobi, Kenya, Sosthenes Bichang'a.

Friday, April 15, 2011

BATA LA MARIPOTA WA KILI TAIFA CUP SOUTH BEACH LEO

WAANDISHI wa habari za michezo, hususan wa mashindano ya Kili Taifa Cup, leo walikuwa na wakati mzuri ambapo walifanyiwa semina na kisha kushiriki michezo, kula na kunywa, kwenye hoteli ya South Beach, Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Michezo waliyoshiriki ni pamoja na soka kwa mashabiki wa timu mbili mashuhuri za Simba na Yanga ambapo mwisho wa mchezo Yanga waliibuka kidedea kwa kushinda bao moja.

Yafuatayo ni matukio ya bata hilo kwenye picha


Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, David Minja akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Simba, .Amri Massare


Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah akikabidhi jezi kwa nahodha wa timu ya mashabiki wa Yanga, Muhidin Sufiani


Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akijibu maswali ya waandishi hao


Waandishi w ahabari za michuano ya Kili Taifa Cup inayotarajiwa kuanza mwezi ujao wakipata darasa

Tuesday, March 29, 2011

DK SHEIN ATAWAZWA KUWA MKUU WA CHUO KIKUU ZANZIBAR 'SUZA'

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein leo ametawazwa rasmi kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar, SUZA, katika sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya Majestic mjini Unguja.

Zifuatazo ni picha mbalimbali za tukio hilo:



Baadhi ya wahadhiri wa chuo hicho wakiwa kwenye maandamano kuelekea eneo la tukio.



Dk. Shein akikabidhiwa kabrasha la vifungu vya sheria vinavyomuwezesha kuwa Mkuu wa chuo hicho



Sasa ni muda muafaka! Dk Shein akivishwa joho kama ishara ya kuwa Mkuu wa chuo hicho baada ya kutawazwa rasmi

PHOTO/SOURCE: STATE HOUSE, ZANZIBAR

DK BILAL AKAGUA MASHAMBA YA MPUNGA YA MTO WA MBU

Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal leo ameingia kwenye siku ya tatu ya ziara yake katika mkoa wa Arusha ambapo anatembelea miradi mbalimbali kwa lengo la kuikagua pamoja na kuizindua mingine.

Miongoni mwa miradi aliyoizindua ni pamoja na ujenzi wa Maabara ya Shule ya Sekondari ya Nanja, wilayani Monduli.

Leo Dk Bilal ametembelea mashamba ya mpunga yaliyopo kwenye mabonde ya mto wa Mbu, wilayani Monduli pamoja na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la maabara ya Shule ya sekondri Nanja, wilayani Monduli. Zifuatazo ni picha mbalimbali zinazoonyesha matukio hayo:



Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal akiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirima kukagua mashamba hayo



Dk Bilal akiangalia mashamba hayo



Dk Bilal akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la maabara ya shule hiyo. Wa mwisho kabisa ni Mbunge wa wilaya hiyo, Edward Lowassa

RITA KUANZA KAMPENI YA KUSAJILI VIZAZI NA VIFO



Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini (RITA), Fillip Saliboko (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam leo kuhusu Kampeni ya Usajili wa Vizazi na Vifo kwa Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam. Mwingine ni Mkurugenzi wa Haki za Kisheria (DLRP), Emmy Hudson

PHOTO/SOURCE: YUSUF BADI

JK AKABIDHIWA RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI



Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete taarifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali na mashirika yake Ikulu, Dar es Salaam jana

PHOTO/SOURCE: STATE HOUSE

MWAKILISHI WA NAKAYAMA AKAGUA MAENDELEO SEKONDARI YA WAMA-NAKAYAMA

Rais wa Shirikisho la Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika (AFRECO) ambaye pia ni Mwakilishi wa Nakayama kutoka nchini Japan, Seneta Tetsuro Yano leo ameitembelea Shule ya Sekondari ya wasichana ya WAMA-Nakayama iliyopo Nyamisati mkoa wa Pwani kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya shule hiyo.

Zifuatazo ni picha mbalimbali zinazoonyesha ziara ya Kiongozi huyo akiwa na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete


Seneta Yano akikabidhi madaftari kwa walimu wa shule hiyo. Kulia ni Mama Salma Kikwete


Sehemu ya wanafunzi wa shule hiyo wakiwa wenye tabasamu wakati wa ugeni wa kiongozi huyo


Seneta Yano na Mama Salma Kikwete wakiwa darasani


Seneta Yano akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi, walimu na wanafunzi wa shule hiyo

PICHA: MAELEZO

UTEPE MWEUPE WATOA SOMO LA UZAZI KWA WABUNGE


Mratibu wa Muungano wa utepe mweupe wa uzazi salama nchini, Rose Mlay akielezea jambo kwa wenyeviti wa kamati mbalimbali za bunge za kudumu pamoja na wajumbe, wakati wa mkutano kuhusu hali ya uzazi nchini uliofanyika Dar es Salaam jana.

Katika mkutano huo mada mbalimbali zinazohusu uzazi salama kwa Mama mjamzito na mimba za utotoni ziliwasilishwa.

NEMC YATOA MILIONI 15 KWA VIKUNDI VYA MAZINGIRA

Baraza la Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC), leo asubuhi limekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 15 kwa vikundi vya mazingira kutoka mikoa mitatu ya Kilimanjaro, Mara na Morogoro kwa ajili ya kusaidia kuendeleza miradi ya mazingira katika maeneo yao.

Vikundi hivyo ni Angaza Women cha Siha mkoani Kilimanjaro, Watu Maji na Mazingira (WAMAMA) cha Tarime mkoani Mara pamoja na Kilombero Group for Community Development (KGCD) ambavyo kila kimoja kimepata shilingi milioni 5.


Wawakilishi wa vikundi hivyo, (Kutoka kushoto) Christina Kulunge wa Morogoro, Lucas Bwana wa Tarime na Mama Mchungaji Joyceline Njama wa Kilimanjaro kwa pamoja wakiangalia mfano wa hundi yao waliyokabidhiwa leo na NEMC

Monday, February 7, 2011

CUF WAANDAMANA KUPINGA SERIKALI KUILIPA DOWANS


Wafuasi wa Chama cha wananchi (CUF) wakiandamana kuipinga Serikali kuilipa kampuni ya kuzalisha umeme ya DOWANS shilingi bilioni 94, Dar es Salaam leo asubuhi. PICHA: YUSUF BADI

WANAFUNZI UDSM WAPIGWA MABOMU YA MACHOZI WAKIDAI SH 10,000 YA 'BOOM'

Askari wa kutuliza ghasia 'ffu' leo mchana wamewavurumishia mabomu wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam muda mfupi baada ya kuisha kwa mkutano wao na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa uliokuwa ukijadili ongezeko la kiwango cha fedha za kujikimu 'Boom' kwa wanafunzi hao.

Muda mfupi baada ya kuondoka kwa waziri huyo, wanafunzi hao walianza kuwaandama askari hao waliokuwa wakiondoka eneo hilo kwa kuwarushia mawe, chupa za maji na vitu vinginevyo, na kuwazomea jambo ambalo lilizua tafrani kubwa baina ya askari na wanafunzi hao na kulazimika kufyatua mabomu ya machozi kwa mfululizo kwa wanafunzi hao waliokuwa wakivurumisha mawe kwa mfululizo.

Hata hivyo askari hao walifanikiwa kutawanya maelfu ya wanafunzi hao waliokuwa wakiwazonga askari hao waliokuwa na magari maalumu aina ya Defender na Land Cruiser, na kuacha wengine wakiwa wamezimia na wengine kujeruhiwa na mabomu hayo.

Awali katika mkutano wao wanafunzi hao na waziri Kawambwa, walimtaka waziri huyo atoe tamko la ongezeko la kiwango cha fedha hizo kutoka shilingi 5,000 ya sasa mpaka 10,000 waliyokuwa wakidai, jambo ambalo lilimpa wakati mgumu waziri huo kulitolea uamuzi wa moja kwa moja, ambapo kila alipokuwa akizungumzia 'mchakato' wanafunzi hao walikuwa wakizomea na kusema "Hatutaki siasa, tunataka elfu kumi tu."

Hata hivyo Waziri Kawambwa alilazimika kuahirisha mkutano huo baada ya hali kuanza kuwa tete pale wanafunzi hao walipoanza kufanya fujo huku wakimlazimisha atoe tamko litakalowaridhisha wanafunzi hao. "Mimi nimewasikia, nitaenda kushauriana na Hazina tuone namna gani tunaongeza kiwango hcho, lakini si elfu kumi kama mnavyodai.." Alisema hivyo waziri Kawambwa na kusababisha maelfu ya wanafunzi hao waliokuwa wakimsikiliza kuanza kupiga kelele kwa kusema "tunatakaa, aashuukee... Tunataakaa, aashuukee..." na ndipo waziri kawambwa alipoufunga mkutano huo na kuondoka huku akiwaacha wanafunzi hao wakiwa na maswali mengi ya kujiuliza.

Muda mfupi baada ya waziri Kawambwa kuondoka eneo hilo, wanafunzi hao walihamishia hasira zao kwa askari wa kutuliza ghasia 'ffu' kwa kuanza kuwavurumishia mawe, chupa za maji na vitu vingine huku wakiwazomea, jambo lililopelekea askari hao kuanza kufyatua mabomu ya machozi kwa mfululizo na kupelekea eneo hilo kugeuka na kuwa la vita, huku vishindo vikubwa vya mabomu hayo vikisikika na kusababisha moshi mwingi kutanda angani.

HABARI PICHANI: