

Rais Jakaya Kikwete akiwasili Lancaster House, jijini London leo kujiunga na viongozi wa nchi mbalimbali katika mkutano wa kujadili mustakabali wa hali ya machafuko nchini Somalia ambayo imekuwa katika misukosuko kwa zaidi ya miaka 20. Jumuiya ya Kimatifa ikiongozwa na Uingereza imedhamiria kumaliza matatizo mbalimbali katika nchi hiyo ikiwemo kutokuwa na Serikali inayoeleweka, Uharamia, Ugaidi pamoja na kujaribu kurudisha amani.
Source: Ikulu
No comments:
Post a Comment