Tuesday, February 21, 2012

MASHINDANO YA KUCHOMA NYAMA: SAFARI LAGER NYAMA CHOMA 2012 YATANGAZA BAA ZILIZOCHAGULIWA DAR ES SALAAM NA MBEYA

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza majina ya baa bora zlizochaguliwa kuingia kwenye mchujo wa awali kwa mikoa ya Dar es Salaam na Mbeya kwenye yale mashindano ya aina yake nay a kuvutia ya kuchoma nyama yajulikanayo kama ‘Safari Lager Nyama Choma 2012’


Jaji Mkuu wa Shindano la Safari Lager Nyama Choma, Douglas Sakibu (kushoto akifafanua jambo wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu baa zilizochaguliwa kushiriki shindano la Safari Lager Nyama Choma 2012. Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.

Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alizitaja baa hizo ambazo ni ishirini ni kama zifuatazo;

DAR ES SALAAM
- Huduma Baa, Rosehill Garden, Kilwa Road Pub, Pentagon Pub, Texedo Garden, Gadafi Square, Angels Pub, Fyataga Bar, Jambo Lee, Hongera Bar, Break Point Bar, Meeda Bar, Titanic Bar, Mangi Bar, Africenter Bar na Twiga.


Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (katikati)akifafanua jambo wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu baa zilizochaguliwa kushiriki shindano la Safari Lager Nyama Choma 2012. Kushoto ni Jaji Mkuu wa shindano hilo, Douglas Sakibu (kushoto) na Jaji Msaidizi,

MBEYA
-Mbeya Carnival, City Pub, 2000 Grocery, Kalembo Bar, Shaba Bar, Makasini Bar, Freepark Bar, Savoy Bar, Double J Bar na Coasini Bar.

No comments:

Post a Comment