Friday, February 24, 2012

MAMIA WAMUAGA MAMA MZAZI WA BLANDINA NYONI

Mamia ya wakazi wa Dar es Salaam wakiwemo viongozi mbalimbali wa ngazi za juu Serikalini wamejitokeza kwenye ibada ya kumuaga Mama mzazi wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Blandina Nyoni, Mama Ester Nyimbo Badi katika Kanisa la Azania front jijini.

Marehemu Ester Nyimbo Badi alisafirishwa leo kwenda Iringa kwa mazishi.



Mwili wa Mama Ester Nyimbo Badi ukiingizwa kwenye gari maalumu kwa ajili ya kusafirishwa kwenda iringa kwa mazishi.

source: Courtesy of Badi

No comments:

Post a Comment