Thursday, February 23, 2012

WAZIRI SAMIA SULUHU ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO ZANZIBAR


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kuhusu upakuaji wa makontena katika bandari ya Zanzibar kwa Mkuu wa Mipango (ZPC), Ali Haji Haji wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo mjini humo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Bandari, Msanifu Haji Mussa na Maofisa wa Bandari ya Zanzibar.




Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Samia Suluhu Hassan akitembelea Bandari ya Zanzibar wakati wa ziara yake ya kuangalia shughuli za Maendeleo mjini humo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa bandari, Msanifu Haji Mussa na Maofisa wa Bandari Zanzibar.

Source: VPO

No comments:

Post a Comment